Powered by Blogger.

On Bloggers

WAFANYABIASHARA WAPINGA MAANDAMANO YA CHADEMA

  Na Mwandishi Wetu, Lindi JUMUIYA ya Wafanyabishara Tanzania (JWT), imepinga uwapo wa maandamano yaliyoitishwa na Chama Cha Demokrasia na M...

 


Na Mwandishi Wetu, Lindi

JUMUIYA ya Wafanyabishara Tanzania (JWT), imepinga uwapo wa maandamano yaliyoitishwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa sababu waathirika wakubwa wa ni wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao kando ya barabara na mitaani.

Maandamano hayo yamepangwa kufanyika Jumatano ya wiki ijayo, Januari 24, 2024, kuanzia Mbezi Luis Standi ya Magufuli kuelekea hadi Ofisi za Umoja wa Mataifa mkoani Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa JWT, Hamis Livembe, akizungumza na waandishi wa habari leo mkoani Lindi, amewataka wanasiasa ambao wana hoja zilizotofautiana na serikali kurudi kukaa mezani ili kupata suluhu badala ya kufanya maandamano hayo.

"Sisi wafanyabishara tunapinga haya maandamano kwasababu sisi ndio waathirika wakubwa kwa kuwa yanapita sehemu zetu za biashara na wao wanapenda kupita sehemu zenye biashara na mikusanyiko ya watu wengi, zinapotokea rapsha maduka yanavunjwa, kufungwa, fujo na siku hiyo bishara zinakuwa haziwezi kufanyika kwa hiyo sisi tunapinga jambo hili," amesema Livembe.

Ametolea mfano maandamano yaliyofanyika nchini Kenya hivi karibuni na kusema walioathirika ni wafanyabishara ambao walishindwa kuendelea na kazi na wengine biashara zao ziliharibiwa.

"Hapa Tanzania nimeambiwa yanataka kuanzia Mbezi Magufuli pale tuna wafanyabishara karibu 2,000 lakini barabara walizochagua kupita kuna watu wanafanyabishara kando ya barabara, kuna mabasi, magari ya abiria, tax na ubber ambazo zinaweza kuathiriwa kama maandamano yatafanyika, hivyo tunashauri wanaioopingana na serikali watafute njia nyingine za kufanya lakini wasisumbue wafanyabishara wetu," amesisitiza Livembe.

COMMENTS

Name

HABARI,6,
ltr
item
MAOKOTO BLOG: WAFANYABIASHARA WAPINGA MAANDAMANO YA CHADEMA
WAFANYABIASHARA WAPINGA MAANDAMANO YA CHADEMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3jB-Jwzf8HMlxOgkLjN0plU_hx8qeyB8Be-LIbghQI71aFcU3AR87-6-cvurPnj8YuBR6ojJDX29RHZzxeJA-FXdB2jv0WWVNEItNK_vuyRYtzdxVy36S18ZydEDYdwDFkAHlEYnqy2z50bXM8raKjO9IN0WPUEwWKMYxc98GciKLDgFWoAozDRTpcbM/s600/WhatsApp%20Image%202024-01-19%20at%2015.28.22.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3jB-Jwzf8HMlxOgkLjN0plU_hx8qeyB8Be-LIbghQI71aFcU3AR87-6-cvurPnj8YuBR6ojJDX29RHZzxeJA-FXdB2jv0WWVNEItNK_vuyRYtzdxVy36S18ZydEDYdwDFkAHlEYnqy2z50bXM8raKjO9IN0WPUEwWKMYxc98GciKLDgFWoAozDRTpcbM/s72-c/WhatsApp%20Image%202024-01-19%20at%2015.28.22.jpeg
MAOKOTO BLOG
https://maokotoblog.blogspot.com/2024/01/wafanyabiashara-wapinga-maandamano-ya.html
https://maokotoblog.blogspot.com/
https://maokotoblog.blogspot.com/
https://maokotoblog.blogspot.com/2024/01/wafanyabiashara-wapinga-maandamano-ya.html
true
1110674963273841250
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS PREMIUM CONTENT IS LOCKED STEP 1: Share to a social network STEP 2: Click the link on your social network Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy Table of Content